Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
1
www.ahlulathaar.com
اإلسالم دين كامل Mwandishi:
اإلمام دمحم األمني الشنقيطي
Imaam Muhammad Amiyn ash-Shanqiytwiy
Tarjama:
Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
2
www.ahlulathaar.com
00- Dibaji ya Uislamu ndio dini kamilifu .......................................................................................................... 3
01- Tawhiyd na kuamini uola wa Allaah ..................................................................................................... 6
01- Tawhiyd na haki pekee ya Allaah kuabudiwa ...................................................................................... 9
01- Tawhiyd na kuamini majina na sifa Zake ............................................................................................ 11
02- Mawaidha ..................................................................................................................................................... 13
03- Tofauti kati ya matendo mema na matendo mabaya ............................................................................. 16
04- Kuhukumu kwa isiyokuwa Shari´ah ........................................................................................................ 19
05- Hali ya jamii .................................................................................................................................................. 22
06- Uchumi .......................................................................................................................................................... 27
07- Siasa ............................................................................................................................................................... 29
08- Nguvu za makafiri juu ya waislamu ......................................................................................................... 33
09- Idadi dhaifu ya waislamu na udhaifu wa nguvu za kijeshi ukilinganisha za makafiri ..................... 34
10- Jamii kutofautiana nyoyo ........................................................................................................................... 39
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
3
www.ahlulathaar.com
00- Dibaji ya Uislamu ndio dini kamilifu
Himdi zote zinamstahikia Allaah, Mola wa walimwengu. Swalah na salaam
zimwendee Mtume wetu Muhammad, familia yake, Maswahabah zake na
wale wenye kuita katika ulinganizi wake mpaka siku ya Qiyaamah.
Amma ba´d:
Huu ni muhadhara niliotoa kwenye msikiti wa Mtume kutokana na ombi la
mfalme wa Marocco. Baada ya hapo baadhi ya ndugu zangu wakanitaka
kuuandaa ili kuueneza. Nikawakubalia kwa kutarajia Allaah atanufaisha
kwao.
Allaah (Ta´ala) amesema:
اللييم لمم م ل م ل ت لم ت ل د نم ت ل
"Leo Nimekukamilishieni dini yenu."1
Siku hiyo ilikuwa ni siku ya ´Arafah. Ilikuwa ni siku ya Ijumaa katika Hajj ya kuaga. Aayah hii tukufu iliteremka na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesimama katika ´Arafah. Baada ya kuteremshwa, aliishi (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) siku thamanini na moja.
Katika Aayah hii tukufu Allaah (Ta´ala) ameweka wazi kwamba
ametukamilishia dini yetu. Hatoipunguza kamwe na wala haitohitajia
nyongeza. Kwa ajili hiyo ndio maana Amefanya utume kumalizika kwa
Mtume wetu - Swalah na salaam ziwaendee wote.
Kadhalika ameweka wazi ya kwamba ameridhia kwetu Uislamu ndio iwe dini
yetu. Ina maana ya kwamba Hatokasirika kwa hilo kamwe. Kwa ajili hiyo
ndio maana amesema kuwa hatoikubali dini nyingine. Amesema:
1 05:03
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
4
www.ahlulathaar.com
نلوت مىت م د اال د م د مديم االمااد د يم مد د ننا يم مي يتقل م م مد مممي يم يل م د مييل م اإللدال م
"Na yeyote anayetaka dini isiyokuwa ya Kiislamu basi haitokubaliwa kwake; naye katika Aakhirah atakuwa miongoni mwa waliokhasirika."2
مت دنن اللد يم دنلم ال نيود اإللدال م
"Hakika dini mbele ya Allaah ni Uislamu."3
Kujengea juu ya kwamba dini imekamilika na hukumu zote ziko waziwazi,
ndio kunafikiwa neema zote katika maisha haya na huko Aakhirah. Ndio
maana Amesema:
م م لم ل ت م ميل ت ل د ل م د
"... na Nimekutimizieni neema Yangu."4
Katika Aayah hii tukufu kuna dalili ya wazi juu ya kwamba Uislamu
haukuacha kitu chochote ambacho viumbe wanahitaji duniani wala Aakhirah,
isipokuwa imekiweka wazi na kukibainisha.
Tutatoa baadhi ya mifano juu ya hilo. Kutabainishwa mambo kumi makubwa
ambayo dunia hii inazunguka juu yake. Mambo hayo yanawahusu
walimwengu duniani na Aakhirah.
La kwanza: Tawhiyd.
La pili: Mawaidha.
La tatu: Tofauti kati ya matendo mema na matendo mabaya.
La nne: Kuhukumu kwa isiyokuwa Shari´ah.
La tano: Hali ya jamii.
La sita: Uchumi.
2 03:85
3 03:19
4 05:03
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
5
www.ahlulathaar.com
La saba: Siasa.
La nane: Nguvu za makafiri juu ya waislamu.
La tisa: Idadi dhaifu ya waislamu na udhaifu wa nguvu za kijeshi
ukilinganisha za makafiri.
La kumi: Jamii kutofautiana nyoyo.
Tutayaangalia matatizo yote haya kupitia Qur-aan.
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
6
www.ahlulathaar.com
01- Tawhiyd na kuamini uola wa Allaah
Kupitia tafiti za kiusomi wa Qur-aan imepata kujulikana kuwa kuna aina tatu
za Tawhiyd:
Ya kwanza: Kumpwekesha Allaah katika uola Wake.
Aina hii ya Tawhiyd inakubaliwa na maumbile ya mtu mwerevu. Amesema
(Ta´ala):
ملم دي ام ملل يم ت منيل م مقم ت ل لمييمقت لتين ال نيوت
"Ukiwauliza: "Ni nani kawaumba?" Bila shaka watasema: "Ni Allaah.""5
بد ت مبلصمارم مممي يتل دجت اللمين مديم الل ميد د ميتل دجت الل ميد م مديم اللميد مممي تلم عم ماألل مرلضد ممني يمل دكت السن ل قت ل ممي يم لزتقت ت مد يم السن ماءد ماأللممل م يمقت ل م م م يم ينقت نم مسمييمقت لت نم ال نيوت األل
"Sema: “Nani anayekuruzukuni kutoka mbinguni na ardhini au nani anayemiliki kusikia na kuona na nani anayemtoa aliye hai kutoka maiti na anayemtoa maiti kutoka aliye uhai na nani anayeendesha mambo?" Watasema: "Ni Allaah". Basi sema: “Je, basi hamumchi?”6
Pindi Fir´awn alipokanusha aina hii pale aliposema:
ممما رم ب الل مالم دنيم
“Ni nani huyo Mola wa walimwengu?”7
alifanya hivo tu kwa sababu ya kiburi na kujifanya ni hamnazo. Dalili ya hilo
ni maneno Yake (Ta´ala):
مرلضد بمصمااد م ءد د ن رم ب السن ما مااد ماألل يـ ت م لمقملل م د ل م مما م نملم ىم
“Hakika umekwishajua kwamba hakuna aliyeteremsha haya isipokuwa Mola wa mbingu na ardhi kuwa ni ushahidi wa kuonekana."8
5 43:87
6 10:31
7 26:23
8 17:102
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
7
www.ahlulathaar.com
قمنيم يل ما م فتست ت ل ظت ل نا م ت ت ا مجمحملت ا بدما ماال يمييل
"Wakazikanusha kwa dhulma na kujivuna na hali kuwa nafsi zao zimeziyakinisha."9
Kwa ajili hiyo Qur-aan ilikuwa ikishuka kwa njia ya kuthibitisha aina hii ya
Tawhiyd kupitia vitu vyenye kuthibitishwa. Mfano wa hilo ni maneno Yake
(Ta´ala):
م د ال نيود مكك
“Je, kuna shaka kuhusiana na Allaah."10
ءء قت ل م مييل م ال نيود مبل دي رم مىت م رم ب ت د ميل
"Sema: “Je, nishike Mola mwingine asiyekuwa Allaah hali Yeye ni Mola wa kila kitu?"""11
مرلضد قت د ال نيوت قت ل ممي رن ب السن ما مااد ماألل
"Sema: “Ni nani Mola wa mbingu na ardhi?” Sema: “Ni Allaah.""12
Hata hivyo aina hii ya Tawhiyd haikuwanufaisha makafiri kitu, kwa kuwa hawakuwa wakimuabudu Allaah (Jalla wa ´Alaa) Yeye peke yake. Amesema (Ta´ala):
ل نيود د ن مىت مبشل د ت نم ممما يت لمديت م ل يم تىت د
"Na wengi kati yao hawamwamini Allaah isipokuwa ni washirikina."13
مما يم ل تلتىت ل د ن لدييتقم د بت وم د م ال نيود زتللفم ـ
“Hatuwaabudu isipokuwa ili watukurubishe kwa Allaah ukaribio."14
9 27:14
10 14:10
11 06:164
12 13:16
13 12:106
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
8
www.ahlulathaar.com
ءد تفم مااتوم دنلم ال نيود يـ ت م م يمقت لت نم ىم
"Wanasema: “Hawa ni waombezi wetu mbele ya Allaah.""15
14 39:03
15 10:18
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
9
www.ahlulathaar.com
01- Tawhiyd na haki pekee ya Allaah kuabudiwa
Aina hii ndio ilikuwa sababu ya magomvi kati ya Mitume na nyumati zao.
Aina hii ya Tawhiyd ndio ilikuwa sababu ya Mitume kutumwa ili
waihakikishe. Kwa ufupi ndio maana ya hapana mungu wa haki isipokuwa
Allaah. Tamko hili limejengwa juu ya misingi miwili: kukanusha na
kuthibitisha.
Ukanushaji unakuja katika kukanusha vyote vinavyoabudiwa badala ya
Allaah. Hili linahusiana na aina zote za ´ibaadah.
Kuthibitisha kunakuja katika kumpwekesha (Jalla wa ´Alaa) katika aina zote
za ´ibaadah kwa mujibu wa zile njia zilizowekwa. Sehemu kubwa ya Qur-aan
inahusiana na aina hii:
ملمقملل بيم م يلنما د ت د تمن ء رنات ن مند ا ل تلت ا ال نيوم ماجل مند ت ا الطنا ت ام
"Hakika Tulituma katika kila ummah Mtume [awaamrishe watu] kwamba: “Mwabuduni Allaah na jiepusheni na miungu ya uongo.""16
ي دلميلود م نوت م دلميـوم د ن موم ما ل تلت ند ممما مرلام لنما مدي قيم ل دكم مدي رنات لء د ن ت ود
"Hatukutuma kabla yako Mtume yeyote isipokuwa Tulimfunulia Wahy ya kwamba: “Hakika hapana mungu wa haki isipokuwa Mimi, basi Niabuduni.""17
لل ت ل م د الل ت يلقم ـ ل نيود يمقملد اال م لسمكم د لطنا ت اد م يت لمدي د فت ل د م مي م ل
"Basi atakayemkanusha mungu wa batili na akamwamini Allaah kwa hakika atakuwa ameshikilia imara kishikilio madhubuti."18
ماال ملل مميل مرلام لنما مدي قيم ل دكم مدي ربات دنما مجم م لنما مدي ت ند ال ن لميـيد آدم ن يت ل ملت نم
"Na waulize wale Tuliowatuma kabla yako miongoni mwa Mitume Wetu: "Je, Tulifanya badala ya Mwingi wa Rahmah miungu mingine iabudiwe?""19
16 16:36
17 21:25
18 02:256
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
10
www.ahlulathaar.com
له يم م ل م ت مبسل د ت نم قت ل د نما ت وم ـ د من م نما دلميـ ت ت ل دلميـوه ماود
"Sema: “Hakika nimefunuliwa Wahy kwamba: "Mungu wenu wa haki ni mungu Mmoja Pekee" - Je, basi simsilimu?""20
Kuna Aayah tele juu ya maudhui hii.
19 43:45
20 21:108
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
11
www.ahlulathaar.com
01- Tawhiyd na kuamini majina na sifa Zake
Aina hii ya Tawhiyd vilevile imejengwa juu ya misingi miwili, kama
Alivyobainisha (Jalla wa ´Alaa).
Wa kwanza: Kuzitakasa sifa Zake (Ta´ala) kushabihiana na za viumbe.
Wa pili: Kuamini yale yote aliyojisifu Mwenyewe na yale aliyomsifu Mtume
Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Mtu anatakiwa kuamini kuwa sifa
hizi ni za kihakika kwa njia inayolingana na utukufu na ukubwa Wake na sio
Majaaz. Ni jambo linalojulikana fika ya kwamba hakuna mjuzi zaidi wa
kumtambua Allaah kama anavyojijua Mwenyewe. Wala hakuna ambaye
anamsifu Allaah kwa kumtambua zaidi baada ya Yeye Mwenyewe kama
Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Allaah (´Azza wa Jall)
amesema juu ya nafsi Yake Mwenyewe:
م م ت ل م ل م ت ممد
“Je, nyinyi mnajua zaidi au Allaah?”21
Amesema kuhusu Mtume Wake:
يه ت وم ـ ممما منطد ت ميد اآلم م ـ دنل ىت م د ن مول
"Na wala hatamki kwa matamanio yake. Hayo ayasemayo si chochote isipokuwa ni Wahy unaofunuliwa kwake."22
Amebainisha (Ta´ala) hali ya kukanusha kufanana aliposema:
ءه لميل م م د ل دود ميل
"Hakuna chochote kinachofanana Naye."
Wakati huo huo akabainisha kuthibitisha sifa kihakika:
مىت م السن ديعت الل مصد ت
21 02:140
22 53:03-04
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
12
www.ahlulathaar.com
"Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona."23
Sentesi ya kwanza ya Aayah inafahamisha kutokanusha. Kunapata kubainika
kupitia Aayah ya kwamba lililo la wajibu ni kuthibitisha sifa kihakika pasi na
kufananisha na wakati huo huo kupinga ufananishaji pasi na ukanushaji.
Amewabainishia viumbe ya kwamba hawawezi kumzunguka (Jalla wa ´Alaa).
Amesema:
م م للد د ل ممما م لفم ت ل م م يتديطت نم بدود د ل نا يم ل م ت مما بيمنيل
"Anajua yale yaliyoko mbele yao na yale yaliyoko nyuma yao na wala wao hawawezi kuizunguka elimu Yake."24
23 42:11
24 20:110
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
13
www.ahlulathaar.com
02- Mawaidha
Wanachuoni wamekubaliana juu ya kwamba Allaah (Ta´ala) hakuteremsha
mawaidha na maonyo makubwa kama utambuzi na elimu. Inahusiana na
mwanaadamu kutambua kuwa Mola wake (Jalla wa ´Alaa) ni mwenye
kumchunga na ni mtambuzi kwa kila kile anachokificha na kukidhihirisha.
Wanachuoni wamepigia mfano wa mawaidha na maonyo haya makuwa.
Wanasema:
Tukadirie kuna mfalme jasiri mwenye kumwaga damu na kuua watu hovyo.
Nyuma yake kuna katili na upange wake mkononi mwenye kumwaga damu.
Pembezoni mwake huyo mfalme kuna wasichana na wakeze. Ni jambo
linawezekana kwa yeyote katika walioko pale kufikiria kumshambulia mmoja
katika wale wasichana au wake zake ilihali ni mwenye kujua anachokifanya
na anamuona? Hapana. Sifa tukufu zaidi zinatajwa katika mnasaba wa Allaah
(´Azza wa Jall) peke yake. Walioko pale wote watakuwa na woga na wenye
kunyenyekea. Kikubwa watachokuwa wanataraji ni amani na usalama.
Ni jambo lisilokuwa na shaka yoyote ya kwamba Allaah (´Azza wa Jall)
anaona na kutambua zaidi kuliko mfalme huyu. Adhabu Yake vilevile ni
kubwa na yenye kuumiza zaidi. Lau watu wa mji wangalijua kuwa mfalme
wao anayajua yale yote wanayoyafanya usiku, basi usiku mzima ungalipita
hali ya kuwa wako na woga na wasingefanya maovu yote.
Amebainisha (Ta´ala) hekima ya kuumba viumbe kwa ajili yake, nayo ni
kuwajaribu na kuwapa mtihani ni nani aliye na matendo mema zaidi.
مرلضد زد نم ن آنما لدنيم يل ت مىت ل م يب ت ل مولسميت م م ن دون جم م لنما مما م م األل
"Hakika Sisi Tumefanya vilioko juu ya ardhi kuwa ni pambo lake ili Tuwajaribu nani miongoni mwao mwenye „amali nzuri zaidi."25
Amesema mwanzoni mwa Suurah "Huud":
مء م مانم م ل توت م م الل ماءد لدييم يل ت م ت ل م ب ت ل مولسميت م م ن مرلضم د اد ن د م ن مىت م الن د م م م السن ما مااد ماألل
25 18:07
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
14
www.ahlulathaar.com
"Yeye ndiye Aliyeumba mbingu na ardhi katika siku sita na „Arshi Yake ikawa juu ya maji ili Akujaribuni nani kati yenu mwenye „amali nzuri zaidi."26
Hakusema "mwenye kutenda ´amali nyingi zaidi". Amesema katika Suurah
"al-Mulk":
الن د م م م الل م لام ماللميما م لدييم يل ت م ت ل م ب ت ل مولسميت م م ن
"Ambaye Ameumba mauti na uhai ili akujaribuni ni nani kati yenu mwenye „amali nzuri zaidi."27
Aayah hizi mbili zinabainisha makusudio ya maneno Yake:
ممما م مقل ت االدين ماإللد م د ن لدييم ل تلت ند
"Na Sikuumba majini na wanaadamu isipokuwa waniabudu."28
Pindi ilipokuwa hekima ya viumbe ipo katika majaribio yaliyotajwa, ndipo
Jibriyl akataka kumuonesha mwanaadamu namna ya kushinda mtihani huo.
Alimwambia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
"Ihsaan ni kitu gani?"
Ihsaan ndio kile viumbe wameumbwa kwa ajili yake ili wajaribiwe nayo.
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akabainisha njia ya Ihsaan hii ni
mawaidha na maonyo haya makubwa na kusema:
"Ni kumuabudu Allaah kama vile unamuona na ikiwa wewe humuoni basi
Yeye anakuona."29
Kwa ajili hiyo ndio maana huwezi kufungua ukurasa katika Qur-aan tukufu,
isipokuwa utakuta mawaidha haya makubwa:
26 11:07
27 67:02
28 51:56
29 al-Bukhaariy (1/18) na Muslim (1/38-39)
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
15
www.ahlulathaar.com
نما اإللد سمانم م يم ل م ت مما يت مال دست بدود يمفلستوت منمليت مقيل م ت دلميلود مديل وم ل د الل مرد لد دذل يم يم مقن الل ت يم مقد يماند ميد الليم دنيد م ميد الشد مال د ملمقملل م مقل قم ديله منا يم لفد ت مدي قيم للء د ن لملم لود رمقدييه م ديله
"Hakika Tumemuumba mwanaadamu na tunajua yale yanayomshawishi nafsi yake na sisi Tuko karibu naye kuliko mshipa wa koo. Pale wanapopokea wapokeaji wawili wanaokaa kuliani na kushotoni. Hatamki kauli yoyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha [kurekodi]."30
ممما تننا مااد دنيم يم منيمقتصنين م ميل د بد د ل ء
"Kisha Tutawasimulia kwa ujuzi [yote waliyoyatenda] na hatukuwa wenye kukosekana."31
نلوت مدي قيت ل نء م م يم ل م ت نم مديل م م ء د ن تننا م ميل ت ل ت ت نا دذل تفدييت نم ديود ممما يم لنت ت مي رنبد كم مدي ممما م ت نت د م لنء ممما يم يل ت مدلدكم م م م ل يم م د ن دي د ما ء مب دنيء مرلضد م م د السن ماءد م م م ل م م مدي ذمـ مد يلقمالد ذمرن ء د األل
"Hushughuliki katika jambo lolote na wala husomi humo chochote katika Qur-aan na wala hamtendi „amali yoyote isipokuwa Tunakuwa ni mashahidi juu yenu mnaposhughulika nayo. Na hakifichiki kwa Mola wako chochote cha uzito wa atomu katika ardhi wala mbinguni na hata kidogo kuliko hicho na hata kikubwa zaidi ya hicho isipokuwa kimo katika Kitabu chenye kubainisha."32
نلوت فت ا مد نيم مسل يم لشت نم ديمابيم ت ل يم ل م ت مما تسد ب نم ممما يت ل دنت نم م م د ين ت ل يم يلنت نم تلت رمىت ل لديمسل م ل د نوت م دي ه بد مااد الصبلت رد م م ود
"Tanabahi! Hakika wao wanageuza vifua vyao ili wamfiche Allaah. Tanabahi! Jueni kuwa wanapojigubika nguo zao Yeye anayajua wanayoyafanya siri na wanayoyatangaza. Hakika Yeye ni mjuzi kwa yaliyomo vifuani."33
Mifano kama hii katika Qur-aan ni mingi.
30 50:16-18
31 07:07
32 10:61
33 11:05
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
16
www.ahlulathaar.com
03- Tofauti kati ya matendo mema na matendo mabaya
Qur-aan tukufu imebainisha kuwa matendo mema ni yale yaliyotimiza sharti
tatu. Ikikosekana sharti moja, basi hayatomfaa kitu mwenye nayo siku ya
Qiyaamah:
Ya kwanza: Kitendo hicho kiwe kinaafikiana na yale aliyokuja nayo Mtume
(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)34. Allaah anasema:
ممما تم ت ت ال نات لت م ت ت هت ممما يم ما ت ل منلوت ما يم ت ا
"Yale anayokupeni Mtume, basi yachukueni, na yale anayokukatazani, yaacheni."35
مني تطدعد ال نات لم يمقملل م ماام ال نيوم
"Atakayemtii Mtume basi kwa hakika amemtii Allaah."36
قت ل دن تن ت ل تد ب نم ال نيوم ما ن د ت ود
"Sema: “Mkiwa mnampenda Allaah, basi nifuateni mimi.""37
ممل آمت ل ت م ماءت م م ت ا آمت مد يم اللد يد مما مل ملذمن بدود ال نيوت
"Je, wanao washirika waliowaamuru dini yale ambayo Allaah hakuyaidhinisha?"38
ممل م م ال نيود يمفل يم ت نم
"Au mnamtungia Allaah uongo?”39
Ya pili: Ifanywe kwa ajili ya Allaah (Ta´ala) peke yake. Amesema:
34 al-Bukhaariy (3/167) na Muslim (3/1343).
35 59:07
36 04:80
37 03:31
38 42:21
39 10:59
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
17
www.ahlulathaar.com
ممما تمد ت ا د ن لدييم ل تلت ا ال نيوم تل دصدنيم لموت اللد يم
"Hawakuamrishwa jengine isipokuwa wamwabudu Allaah hali ya kumtakasia Yeye dini."40
منل م ت نم م نلم الل تسل د دنيم قت ل دود م مافت دنل مصميل ت رمبد م ما م يم لمء مظدي ء قت د قت ل دود تمد لات منل م ل تلم ال نيوم تل دصنا لنوت اللد يم م تمد لات ألدلدكم ىت م قت ل دنن االمااد د يم الن د يم مسد ت ا م فتسم ت ل م مىل دي د ل يم لمم اللقديمامم د ال نيوم م ل تلت تل دصنا لنوت د يد ما ل تلت ا مما د يل ت مد ي ت دود م م ذمـ
االتسل مانت الل ت دنيت
"Sema: “Hakika mimi nimeamrishwa nimwabudu Allaah hali ya kumtakasia Yeye dini na nimeamrishwa kuwa niwe wa kwanza wa waislamu.” Sema: “Hakika mimi nachelea nikimwasi Mola wangu nitapata adhabu ya siku kubwa." Sema: "Allaah Pekee ndiye ninayemwabudu hali ya kumtakasia Yeye dini. Basi abuduni mnayotaka badala Yake." Sema: “Hakika waliokhasirika ni wale waliokhasiri nafsi zao na ahli zao siku ya Qiyaamah." Tanabahi! Huko ndiko kukhasirika kwa wazi kabisa.""41
Ya tatu: Iwe imejengwa juu ya ´Aqiydah sahihi. Kitendo ni kama sakafu na
´Aqiydah ni kama msingi. Amesema (Ta´ala):
مممي يم ل م ل مديم الصنالدمااد مدي ذم م ء م ل ت م ـ
"Atakayefanya mema akiwa mwanamume au mwanamke... "
Amefunganisha yote hayo kwa kusema:
مىت م مت لمديه
"... hali ya kuwa ni muumini."42
Upande mwingine amesema kuhusu kafiri:
نما د مـ مما م د ت ا مديل م م ء مجم م لنماهت ىم ماءن منن ت رنا مقملدمل
"Tutayaendea yale waliyoyatenda katika ´amali zao, Tuzifanye kama mavumbi yaliyotawanyika."43
40 98:05
41 39:11-15
42 04:124
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
18
www.ahlulathaar.com
موم د م مما منيم ت ا دي ما م م د ه منا ما ت ا يم ل م ت نم ت لميـ دكم الن د يم لميل م آمت ل د اال د م د د ن الننارت
"Hao ndio wale ambao hawatokuwa na chochote Aakhirah isipokuwa Moto na yataporomoka yale waliyoyafanya duniani nani yenye kubatilika yale waliyokuwa wakiyatenda."44
Kuna Aayah nyingi mfano wa hizo.
43 25:23
44 11:16
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
19
www.ahlulathaar.com
04- Kuhukumu kwa isiyokuwa Shari´ah
Qur-aan imebainisha kuwa kitendo kama hichi ni kufuru na shirki. Pindi
shaytwaan alipowazungumzisha makafiri wa Makkah walimuuliza Mtume
(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni nani mwenye kusababisha kondoo
nyamafu kuwa maiti, akasema: "Allaah." Ndipo akawafanya wamuulize: "Vile
mnavyochinja kwa mikono yenu ni halali na vile anavyochinja Allaah kwa
mkono wake mtukufu ni haramu?" Kwa hivyo nyinyi ni bora kuliko Allaah?"45
Ndipo Allaah akateremsha:
لديمااد د ل لديتجما دلت ت ل م م مل ت ت ا دنا مل ت ل م د اال ت ال نيود م ميلود م د نوت لمفدسل ه م دنل م م ل ت ت ىت ل د ن ت ل لم تشل د ت نم م دنن الشنيما دنيم لميت وت نم د مـ م ل
"Wala msile katika wale wasiotajiwa jina la Allaah - kwani huo ni ufasiki. Hakika mashaytwaan wanadokeza marafiki wao wa ndani ili wabishane nanyi. Na mtakapowatii hakika mtakuwa washirikina."46
Katika Aayah hii Allaah (Jalla wa ´Aaa) anaapa ya kwamba yule ambaye
atamtii shaytwaan katika Shari´ah yake na kuhalalisha nyamafu ya kwamba ni
mshirikina. Inahusiana na shirki kubwa yenye kumtoa mtu katika Uislamu.
Haya ni kwa maafikiano ya waislamu. Allaah atawatweza wenye kuyafanya
hayo na kusema:
ا د مااه مبسل مقدي ه د نوت لم ت ل ملت ك مب دنيه م مند ا ل تلت ود م مل م ل ملل دلميل ت ل م بميد ممم من ن يم ل تلت ا الشنيلطمانم يـ م ىم
“Je, Sijakukuahidini enyi wana wa Aadam kwamba: “Msimwabudu shaytwaan, hakika yeye kwenu ni adui wa wazi na kwamba [badala yake] mniabudu Mimi Pekee - hii ndio njia iliyonyooka."47
Amesema (Ta´ala) kumwambia Ibraahiym:
م مبم د م يم ل تلد الشنيلطمانم
“Ee baba yangu! Usimwabudu shaytwaan."48
45 Abu Daawuud (3/245), at-Tirmidhiy (5/246), an-Nasaa’iy (7/237) na Ibn Maajah (2/1059).
46 06:121
47 36:60-61
48 19:44
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
20
www.ahlulathaar.com
Bi maana kwenye kumfuata katika kuweka kufuru na maasi. Amesema:
ا ثن م دن ملل ت نم د ن ميلطماون من د لن دن ملل ت نم مدي ت دود د ن دوم
"Hawaombi badala Yake isipokuwa [miungu ya] kike na hawaombi isipokuwa shaytwaan muasi."49
Bi maana hakuna jengine walichokuwa wakiabudu isipokuwa shaytwaan. Hilo lilipitika kwa kuchukua Shari´ah zao. Amesema (Ta´ala):
لدكم زم نيم لد م د ء مد يم الل تشل د دنيم قيم ل م م ل م دىد ل ت م مااتىت ل م م مـ
"Na hivyo ndivyo washirikina wengi walivyopambiwa na washirika wao [wanaowaabudu] kuua watoto wao ili wawateketeze."50
Amewapa jina "washirika" kwa kuwa waliwatii katika maasi ya kuwaua
watoto wao.
اانم ت ا مول مارمىت ل مرتىل ما يم ت ل مرل م ن مد ي ت ند ال نيود
"Wamewafanya marabi wao na watawa wao kuwa ni miungu badala ya Allaah."51
Pindi ´Adiyy bin Haatim (Radhiya Allaahu ´anh) alipomuuliza Mtume (Swalla
Allaahu ´alayhi wa sallam) juu ya Aayah hiyo, Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi
wa sallam) akasema kwamba kuwafanya marabi na watawa miungu badala
ya Allaah maana yake ni kuwafuata katika kuhalalisha yale Aliyoharamisha
Allaah na kinyume chake52. Hili ni jambo ambalo hakuna tofauti juu yake.
فت ت ا بدود م مل يم م د م الن د يم يمنل ت ت نم م ين ت ل ممنت ا بدما ت ندلم دلميلكم ممما ت ندلم مدي قيم ل دكم ت د لت نم من يم محما م ت ا د م الطنا ت اد مقملل تمد ت ا من م لا م ت د لت الشنيلطمانت من تيد ن ت ل ضم م ن بم ديلن
49 04:117
50 06:137
51 09:31
52 at-Tirmidhiy (05/259) na amesema:
"Hadiyth hii ni geni."
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
21
www.ahlulathaar.com
"Je, huoni wale wanaodai kwamba wao wameamini yaliyoteremshwa kwako na yale yaliyoteremshwa kabla yako wanataka wahukumiane kwa Twaaghuut na hali wameamrishwa wayakanushe. Na shaytwaan anataka awapoteze upotofu wa mbali kabisa."53
مممي نل يمل ت بدما م نملم ال نيوت م ت لميـ دكم ىت ت الل ما د ت نم
"Na yeyote asiyehukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio makafiri."54
للم د م يم مييل م ال نيود مبيل م دي وم م نا مىت م الن د م نملم دلميل ت ت الل د ما م متفمصن ن نماىت ت الل د ما م يم ل م ت نم م نوت متنيمننله مد ي رنبد كم د م م مالن د يم يمييل م ت مين مديم الل ت ل مد يم
“Je, nitafute hakimu asiyekuwa Allaah Naye ndiye Kakuteremshieni Kitabu kilichopambanuliwa waziwazi?” Na wale Tuliowapa Kitabu wanajua kwamba kimeteremshwa kutoka kwa Mola wako kwa haki. Basi usije kuwa miongoni mwa wanaotia shaka."55
قنا م ملل ن لل مىت م السن ديعت الل م دي ت ن مت ملد لم لد م د ما دود م من ل م د م ت رمبد كم د
"Na limetimia neno la Mola wako kwa ukweli na uadilifu - hakuna mwenye kuyabadilisha maneno Yake. Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua."56
Ukweli ni pindi inapokuja katika maelezo na uadilifu pindi inapokuja katika
hukumu.
ممميل مولسميت مديم ال نيود وت ل نا لد قم لمء ت قدنت نم م محت ل م االماىد دين د يم يل ت نم
"Je, wao wanataka hukumu za kijahiliya? Na nani mbora zaidi kuliko Allaah katika kuhukumu; [yanafahamika haya] kwa watu wenye yakini."57
53 04:60
54 05:44
55 06:114
56 06:115
57 05:50
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
22
www.ahlulathaar.com
05- Hali ya jamii
Hapa Qur-aan imemponya mgonjwa na kuangaza njia. Tazama
inavyomuamrisha yule kiongozi mkubwa kuiangalia jamii yake:
نماومكم لد ميد ا ين يم مكم مديم الل ت لمدندنيم فد ل جم ما ل
"Na inamisha ubawa wako kwa anayekufuata miongoni mwa waumini."58
ممل د ملم ل تن م مظا م دي م اللقم ليد م فميب ا مديل وم للدكم م د ما رم لم ء مد يم ال نيود لدن م آمت ل ما ل ت منيل ت ل ماال يم لفد ل آمت ل م ما درلىت ل د األل
"Basi ni kwa sababu ya rehema kutoka kwa Allaah umekuwa mpole kwao. Na lau ungelikuwa mkali, mwenye moyo mgumu, wangelikukimbia. Basi wasamehe na waombee maghfirah na washauri katika mambo."59
Tazama namna inavyosema kuiambia jamii ifanye nini na watawala wake:
ممل د مدن ت ل م م يب ما الن د يم ممنت ا م دي ت ا ال نيوم م م دي ت ا ال نات لم م ت د األل
"Enyi mlioamini! Mtiini Allaah na mtiini Mtume na wale wenye madaraka katika nyinyi."60
Tazama inavyosema kumwambia mtu anachotakiwa kufanya na jamaa zake kama mfano wa watoto na mke:
ا ه ن يم لصت نم ال نيوم مما ممم مىت ل م يمفل م ت نم لم ظه د اد م ه د م رنا مقت تىما النناست ماللدجمارم ت م مييل ما مم م م م يب ما الن د يم ممنت ا قت ا م فتسم ت ل م مىل دي ت ل وم مما يت لمم ت نم
"Enyi mlioamini! Jikingeni nafsi zenu na ahli zenu na Moto ambao kuni zake ni watu na mawe. Wanausimamia Malaika wakali na wenye nguvu hawamuasi Allaah kwa yale Anayowaamrisha na wanafanya yale wanayoamrishwa."61
Tazama namna inavyomuamrisha mtu awe kwa jamaa zake na kwamba
anatakiwa kusamehe na kupuuza endapo watafanya kitu kisichokuwa na
58 26:215
59 03:159
60 04:59
61 66:06
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
23
www.ahlulathaar.com
uzito. Kwanza inamwamrisha awe ni mwenye kuchunga baada ya hapo
apuuze na kusamehe:
ي ه م م يب ما الن د يم ممنت ا دنن مديل مزل ماجد ت ل م م ل م د ت ل ملت ا لن ت ل ماول مرت ىت ل م دن يم لفت ا م مصلفمحت ا م يم لفد ت ا م دنن ال نيوم مفت ره رنود
"Enyi mlioamini! Hakika miongoni mwa wake zenu na wana wenu [kuna ambao] ni maadui kwenu, basi tahadharini nao! Iwapo mtasamehe na mkapuuza na mkayafutilia mbali, basi hakika Allaah ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu."62
Tazama inavyomuamrisha mtu binafsi katika jamii namna wanavyotakiwa
kutaamiliana:
شماءد مالل تن م د مالل يم ليد سماند م د ماءد ذد اللقت لبمـ م يمنيل م ـ ميد اللفمحل لد ماإللدول لل ملل م دظت ت ل لم م ن ت ل م م ن ت نم دنن ال نيوم ملمت ت د
"Hakika Allaah anaamrishia uadilifu na wema na kuwapa [mahitajio na msaada] ndugu wa karibu na Anakataza machafu na maovu na dhuluma. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumbuka."63
م م تممسنست ا م م يم ل مي بين ليت ت بيم لينا م م يب ما الن د يم ممنت ا اجل مند ت ا م د نا مد يم الظنيد دنن بيم ل م الظنيد دثله
"Enyi mlioamini! Jieupusheni sana kuwa na dhana [mbaya], kwani hakika baadhi ya dhana ni dhambi. Na wala msifanyiane ujasusi na wala wasisengenyane baadhi yenu wengine."64
ييل نا مد نيل تين ييل نا مد نيل ت ل م م دسماءه مد ي د سماءء مسم ـ من م تين م م م يم ل دنت ا م م يب ما الن د يم ممنت ا م مسل م ل قيم لمه مد ي قيم لمء مسم ـ من م ت ت ا ممللقما د ألل يماند م فتسم ت ل م م يمنمابيمنت ا د ال ت اللفتست قت بيم للم اإللد مممي نل يم تيل م ت لميـ دكم ىت ت الظنالد ت نم بد ل م ا د
"Enyi mlioamini! Wanaume wasiwadharau wanaume wenzao - huenda wakawa bora kuliko wao - na wala wanawake wasiwadharau wanawake wenzao - huenda wakawa bora kuliko wao. Na wala msikashifianeni na wala msiitane kwa majina ya kejeli. Ubaya ulioje kutumia jina la ufasiki baada ya kwishaamini. Na yeyote asiyetubu, basi hao ndio madhalimu."65
ثلد مالل تلل ماند م يم ما م ت ا م م الل دد مال ينقل م ـ م م يم ما م ت ا م م اإللد
62 64:14
63 16:90
64 49:12
65 49:11
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
24
www.ahlulathaar.com
"Saidianeni katika wema na kumcha Allaah na wala msisaidiane katika dhambi na uadui."66
د نما الل ت لمدنت نم د ل م ه
"Hakika waumini ni ndugu."67
نيم ت ل م ممل تىت ل ت رم ـ بيمييل
"Na jambo lao hushauriana baina yao."68
Pale ilipokuwa jamii haiwezi kuepuka vikwazo na vipingamizi na wanahitaji
dawa ya kutibu maradhi haya yaliyoenea, ndipo Akabainisha (Ta´ala) dawa
sehemu tatu katika Kitabu Chake. Kikwazo cha mtu kinatibiwa kwa njia ya
kwamba mtu asirudishe ubaya ule ule kwa yule aliyemfanyizia. Badala yake
mtu anatakiwa kulikabili tatizo hilo kwa kutangamana naye kwa uzuri. Ama
kuhusu majini, mtu anaweza kujikinga nayo kwa kumuomba Allaah kinga
kutokamana na wao.
Sehemu ya kwanza: Ameeleza (Ta´ala) dawa dhidi ya kikwazo cha
mwanaadamu mwishoni mwa Suurah "al-A´raaf" na kusema:
لل ت لفد م م ل دضل ميد االماىد دنيم ت د الل مفل م م لمت ل د
"Shikamana na usamehevu na amrisha mema na jiepushe na wajinga."69
Kuhusu vikwazo vya majini amesema:
ل نيود د نوت مديعه م دي ه م دمنا مننم مننكم مديم الشنيلطماند يمنل ه ماال م د ل د
"Na pindi utakapokuchochea uchochezi kutokana na shaytwaan, basi jikinge na Allaah. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia na ni mjuzi."70
66 05:02
67 49:10
68 42:38
69 07:199
70 07:200
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
25
www.ahlulathaar.com
Sehemu ya pili: Katika Suurah "al-Mu´minuun" amesema kuhusu kikwazo
cha mwanaadamu:
يم مولسميت السنيد م م لن د ىد فت نم ا ل معل د نمليت م ل م ت بدما مصد
"Ondosha maovu kwa njia [ya kufanya] yale yaliyo mema zaidi. Sisi Tunajua zaidi yale wanayoyaelezea."71
Upande mwigine amesema kuhusu majini:
مقت رن د م ت ذت بدكم مديل ممنمااد الشنيما دنيد م م ت ذت بدكم رم د من يمليت ت ند
"Sema: “Mola wangu! Najikinga Kwako kutokana na uchochezi wa mashaytwaan na najikinga Kwako Mola wasinihudhurie.""72
Sehemu ya tatu: Katika Suurah "Fuswswilat" amebainisha (Ta´ala) zaidi ya
kwamba dawa hii ya kimbingu inaponya maradhi haya ya kishaytwaan.
Kadhalika akabainisha kuwa sio kila mtu anapata dawa hii ya kimbingu.
Hakuna mwenye kuipata isipokuwa tu yule mwenye bahati kubwa. Amesema
kuhusu hilo katika Aayah ifuatayo:
ك مدي ه ممما يت مقناىما د ن الن د يم م يم ت ا م م مسل م د اللمسمنم ت م م السنيد م ت ا م ه م م نوت م د نموت ملم نمكم مبيمييل يم مولسميت م دذما الن د بيمييللن د ىد ا ل معل د
ممما يت مقناىما د ن ذت وم ء مظدي ء
"Na wala haulingani sawa wema na uovu. Lipiza [uovu ulilotendewa] kwa ambalo ni zuri zaidi; tahamaki yule ambaye baina yako na baina yake kuna uadui atakuwa kama ni rafiki wa ndani. Hawatopewa sifa hii isipokuwa wale waliovuta subira, na hapewi hayo isipokuwa mwenye fungu kubwa."73
Kuhusu kikwazo cha shaytwaan amesema:
ل نيود د نوت ىت م السن ديعت الل م دي ت م دمنا مننم مننكم مديم الشنيلطماند يمنل ه ماال م د ل د
71 23:96
72 23:97-98
73 41:34-35
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
26
www.ahlulathaar.com
"Na utakapokuchochea uchochezi kutoka kwa shaytwaan, basi omba kinga kwa Allaah. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia, Mjuzi."74
Sehemu nyingine amebainisha kuwa upole na ulaini huu inahusiana tu na
muumini na si kafiri. Amesema:
مسم لفم مل د ال نيوت بدقم لمء يتد يب ت ل ميتد ب موت مذدلن ء م م الل ت لمدندنيم م دنن ء م م الل ما د د يم
"... basi Allaah Atawaleta watu [badala yao] atakaowapenda nao watampenda, wanyenyekevu kwa waumini, washupavu kwa makafiri."75
نيم ت ل مبم نله رنات لت ال نيود لناءت م م الل تفنارد رت مماءت بيمييل مالن د يم مم موت م د
"Muhammad ni Mtume wa Allaah. Na wale walio pamoja naye ni wakali zaidi kwa makafiri; wanahurumiana baina yao."76
ب جماىدلد الل تفنارم مالل تنما دقدنيم ما ل ت ل م ميل د ل م م يب ما النن د
"Ee Nabii! Pambana Jihaad na makafiri na wanafiki na kuwa mgumu kwao."77
Kuweka ukali mahali kunatakiwa upole, ni upumbavu na uzembe. Kuweka
upole mahali kunatakiwa ukali, ni udhaifu na kutoweza.
Kunaposemwa "upole", sema kuwa upole una nafasi yake
Upole wa kijana isipokuwa nafasi yake ni ujinga
74 41:36
75 05:54
76 48:29
77 09:73
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
27
www.ahlulathaar.com
06- Uchumi
Qur-aan imebainisha misingi ya kiuchumi ambayo vitaga vyote vinarejea
kwayo, mambo ya kiuchumi yanarudi katika misingi miwili:
Wa kwanza: Njia nzuri ya kuchuma pesa.
Wa pili: Njia ya kuzitumia.
Tazama jinsi Kitabu cha Allaah kinavyombainishia mwanaadamu namna
anavyotakiwa kuchuma pesa kwa njia inayolingana na marua na dini.
Amesema:
مرلضد مابيل يم ت ا مدي ميل د ال نيود يم د الصن م ت ما مشد ت ا د األل م دذما قتيد
"Na inapomalizika swalah, tawanyikeni katika ardhi na tafuteni fadhila za Allaah."78
مرلضد يم يل يم ت نم مدي ميل د ال نيود م م ت نم ميل دبت نم د األل
"Na wengine wanasafiri katika ardhi wanatafuta fadhila za Allaah."79
لميل م م ميل ت ل جتنمااه من يم يل يم ت ا ميل ن مد ي رنبد ت ل
"Hapana kwenu dhambi kutafuta fadhila toka kwa Mola wenu."80
د ن من م ت نم تدمارم ن مي يم ماضء مد ن ت ل
"Isipokuwa iwe biashara kwa kuridhiana baina yenu."81
م موم ن ال نيوت الل يميلعم
"Allaah Amehalalisha biashara."82
78 62:10
79 73:20
80 02:198
81 04:29
82 02:275
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
28
www.ahlulathaar.com
م ت ت ا دنا مند ل ت ل وم م ن ميد نا
"Kuleni katika mlivyopata ngawira [hivyo ni] halali vizuri."83
Tazama namna inavyoamrisha utumiaji wa uchumi:
م م تمل م ل ملمكم مم ل ت لم ن د مـ تنتقدكم م م يم لستطل ما ت ن الل مسل د
"Na wala usifanye mkono wako kama uliofungwa shingoni mwako [kama bakhili] na wala usiukunjue wote kabisa [ukatoa kwa fujo]."84
لدكم قيم مامنا م ذمـ مالن د يم دذما م فمقت ا مل تسل د ت ا م مل يمقل يت ت ا م مانم بيمنيل
"Na wale ambao wanapotoa huwa hawafanyi israfu na wala hawafanyi uchoyo na wanakuwa wastani baina ya hayo."85
قت ل دي د ما دثله م د ه مممنما دعت لد نناسد م دثلت ت ما م ل يم ت مدي ينفل د د ما مسل ملت مكم ميد االم ل د مالل ميلسد د
"Wanakuuliza kuhusu mvinyo na kamari. Sema: “Katika viwili hivyo mna dhambi kubwa na mna manufaa [fulani] kwa watu. Na dhambi yake viwili hivyo ni kubwa kuliko manufaa yake." Na wanakuuliza nini watoe. Sema: “Yaliyokuzidieni.""86
Tazama namna inavyokataza utumiaji wa haramu:
نن م مسميتنفدقت يم ما ثتن م ت نت م ميل د ل ومسل م ن ثتن يت ل م ت نم دنن الن د يم مفم ت ا تنفدقت نم ممل ماآمت ل لديمصتلب ا مي ام دي د ال نيود مالن د يم مفم ت ا د مـ جم م يتلشم ت نم
"Hakika wale waliokufuru wanatoa mali zao ili wawazuie [watu] kutokamana na njia ya Allaah. Basi watazitoa, kisha itakuwa ni majuto juu yao, kisha watashindwa. Na wale waliokufuru watakusanywa kwenye Moto."87
83 08:69
84 17:29
85 25:67
86 02:219
87 08:36
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
29
www.ahlulathaar.com
07- Siasa
Qur-aan imebainisha misingi yake, kuangaza alama zake na kuweka wazi njia
zake. Kuna aina mbili ya siasa: ya nje na ya ndani.
Kuhusu siasa ya nje, ni yenye kuzunguka katika misingi miwili:
Wa kwanza: Kuandaa nguvu ya kutosha ili kujiweka tayari na adui. Amesema
(Ta´ala) kuhusu msingi huu:
اد االميل د يت لىد ت نم بدود ملت ن ال نيود م ملت ن ت ل م م دلب ا آمت منا اال مطم ل ت مد ي قيت ن ء ممدي رد م
"Na waandalieni nguvu zozote mziwezazo na farasi waliofungwa tayari [kwa vita] muwaogopeshe kwayo maadui wa Allaah na maadui zenu."88
Wa pili: Umoja sahihi na wenye kuenea kwa ajili ya nguvu hiyo. Amesema
(Ta´ala):
م ل د ال نيود جمدي نا م م يمفم نقت ا ما ل مصد ت ا بد
"Shikamaneni nyote pamoja kwa kamba ya Allaah na wala msifarikiane."89
ىميم رديت ت ل م م يمنمازم ت ا يم يمفلشم ت ا م م ل
"Na wala msizozane, mtavunjikwa moyo na zikatoweka nguvu zenu."90
Qur-aan imebainisha yenye kufuatia hayo katika kufanya mkataba wa amani
na kukata mkataba mambo yakihitajia kufanya hivo. Amesema (Ta´ala):
لمىت ل د مـ متلن دد ل م م دب ا دلميل د ل م ل
"Watimizieni ahadi yao mpaka muda wao [utimie]."91
م ما اال يمقمامت ا لم ت ل ماال مقدي ت ا آمت ل
88 08:60
89 03:103
90 08:46
91 09:04
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
30
www.ahlulathaar.com
"Wakikunyokeeni [kwa uzuri], nanyi wanyokeeni [kwa uzuri]."92
يما م ن ما د ل دلميل د ل م م ـ ام ماءء دنن ال نيوم م يتديب االماادندنيم م دمنا امما مين مدي قيم لمء د
"Na kama ukihofu khiyana kwa watu [mliofanya nao ahadi], basi watupilie ahadi yao kwa usawa. Hakika Allaah hapendi makhaini."93
م ل مد منن ال نيوم بم د ءه مد يم الل تشل د دنيم مرمات لتوت م مذمانه مد يم ال نيود مرمات لدود د م النناسد يم لمم اللم د األل
"Na ni tangazo kutoka kwa Allaah na Mtume Wake kwa watu siku ya Hajj kubwa kwamba: Allaah na Mtume Wake wamejitenga mbali na washirikina."94
Vilevile Ameamrisha kuwa makini na kuhadhari na njama zao na kutumia
kwao fursa mbio mbio wakipata namna ya kufanya hivo:
رم ت ل م م يب ما الن د يم ممنت ا ت ت ا ود ل
"Enyi mlioamini! Chukueni tahadhari."95
رمىت ل م مال دحم يم ت ل ملليم ل ت ت ا ود ل
"Nao washike hadhari na silaha zao."96
Kuhusu siasa ya ndani, mambo yake yanarudi katika kueneza amani na
utulivu ndani ya jamii, kuzima dhuluma zote na kumpa kila mmoja haki yake.
Siasa ya ndani imejengwa juu ya nukta sita kubwa:
Ya kwanza: Dini. Shari´ah imekuja kuhifadhi suala hili. Mtume (Swalla
Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
"Mwenye kubadili dini yake muueni."97
92 09:07
93 08:58
94 09:03
95 04:71
96 04:102
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
31
www.ahlulathaar.com
Hapo kuna matishio makali kwa yule mwenye kutaka kuibadili dini yake.
Ya pili: Nafsi. Ili kuilinda nafsi, Allaah ameweka kisasi katika Kitabu Chake:
يما ه ملم ت ل د اللقدصمااد وم
"Na mtapata katika [kulipiza] kisasi uhai."98
ت ديم م ميل ت ت اللقدصماات د اللقم يل م
"Mmewekewa Shari´ah kulipa kisasi katika waliouawa."99
مممي قت د م ممظل ت منا يمقملل جم م لنما لد ملديد ود ات لطماون
"Na atakayeuliwa kwa kudhulumiwa, basi Tumemfanya msimamizi wake awe na mamlaka."100
Ya tatu: Akili. Qur-aan imeteremsha mambo yenye kuihifadhi. Amesema
(Ta´ala):
مت ردجل ه مد يل م م د الشنيلطماند ماجل مند ت هت لم م ن ت ل يتفل دحت نم مزل م م صما ت ماألل م م يب ما الن د يم ممنت ا د نما االم ل ت مالل ميلسد ت ماألل
"Enyi mlioamini! Hakika ulevi na kamari na [kuabudu] masanamu, na kutazamia kwa mishale ya kupigia ramli - vyote hivyo ni uchafu katika matendo ya shaytwaan. Basi jiepusheni navyo mpate kufaulu."101
Katika Hadiyth imekuja:
"Kila chenye kulevya ni haramu. Ikiwa kiwango kikubwa kinalewesha, basi
kiwango chake kichache pia ni haramu."102
97 al-Bukhaariy (4/21).
98 02:179
99 02:178
100 17:33
101 05:90
102 Ibn Maajah (2/1124). Kuhusu sehemu yake ya kwanza ”Kila chenye kulevya ni haramu”, iko katika
al-Bukhaariy (5/108) na Muslim (3/1585).
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
32
www.ahlulathaar.com
Kwa ajili ya kuihifadhi akili, ni wajibu kumuadhibu mnywa pombe.
Ya nne: Nasabu. Kwa ajili ya kuihifadhi, Allaah ameweka adhabu kwa ajili ya
uzinifu:
لء مد نيل ت ما مداام م جم للم ء الننا ديم ت مالنناود ماجل دلت ا ت ن ماود
"Mzinifu mwanamke [asiyeolewa] na mzinifu mwanamme [asiyeoa], mpigeni kila mmoja katika wao mijeledi mia."103
Ya tano: Heshima. Kwa ajili ya kulinda heshima, Allaah ameweka ya kwamba yule mwenye kumtuhumu kwa uongo mtu uzinzi apigwe bakora thamanini:
اءم ماجل دلت ىت ل ثمما دنيم جم للم ن صمنمااد ثتن مل مل ت ا دمرلبيم م د ت ملم مالن د يم يم لمت نم الل تحل
"Na wale wanaowasingizia wanawake watwaharifu [kuwa wamezini] kisha hawaleti mashahidi wanne, basi wapigeni mijeledi themanini."104
Ya sita: Mali. Kwa ajili ya kuilinda, Allaah ameweka kukata mkono wa mwizi:
مالسناردقت مالسناردقم ت ماقلطم ت ا م للد يم ت ما جمنماءن بدما مسم ما م ما ن مد يم ال نيود
"Mwizi mwanamume na mwizi mwanamke wakateni mikono yao - ni malipo kwa yale waliyoyachuma ndio adhabu ya mfano kutoka kwa Allaah."105
Mpaka hapa inapata kubainika wazi wazi ya kwamba Qur-aan inaidhamini
jamii maslahi yote, sawa maslahi ya ndani na ya nje ya nchi.
103 24:02
104 24:04
105 05:38
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
33
www.ahlulathaar.com
08- Nguvu za makafiri juu ya waislamu
Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)
walilihoji tatizo hili katika kipindi cha uhai wake. Ndipo Allaah (Jalla wa
´Alaa) akatoa jibu la kimbingu kwa maswali yote. Pindi waislamu
walipofikwa na yakufikwa katika siku ya Uhud, wakahoji tatizo hili.
Wakasema:
"Ni vipi washirikina watatushinda na kututawala ilihali ni sisi ndio tuko
katika haki na wao wako katika batili?"
Allaah akawajibu na kusema:
ا يـ م ي م ه قملل م م يل ت مد يل مييل ما قيت ل ت ل مننـ ىم قت ل ىت م مديل دنلد م فتسد ت ل م ملم نا م مابيم ل ت مبصد
"Nyinyi - ulipokusibuni msiba ambao nyinyi mmekwisha watia mara mbili mfano wa huo - mnasema: “Umetoka wapi huu?” Sema: “Huo ni kutoka kwenu wenyewe.""106
هت دذل متسب يم ت ددذل دود قم ت ت ال نيوت م للم ممل د م مصمييل ت مد ي بيم للد مما مرما ت منا تد ب نم ملمقملل ملم مدن ت مني وم نـ دذما مشد ل ت ل م يمنمازم ل ت ل د األل ثتن م م م ت ل منيل ت ل لدييم يل م ديم ت ل ت د لت اللب يليما ممدن ت مني ت د لت اال د م م
"Hakika Allaah amekwisha kusadikishieni ahadi Yake mlipowaua vikali kwa idhini Yake mpaka mliposhindwa na mkazozana katika amri na mkaasi baada ya Yeye kukuonyesheni yale mnayoyapenda. Miongoni mwenu wako wenye kutaka dunia na miongoni mwenu wako wenye kutaka Aakhirah. Kisha akakugeuzeni nyuma mbali nao [hao maadui] ili Akujaribuni."107
Katika jibu hili la kiungu akabainisha kuwa makafiri kushinda ni kwa sababu
ya waislamu wenyewe. Yote hayo yamepitika baada ya wao kuwa na tofauti
na kuasi amri ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kuyapupia
mambo ya kidunia. Washambuliaji waliokuwa juu ya mlima walikuwa
wakiwazuia makafiri kuwashambulia waislamu kwa upande wa nyuma.
Pindi washirikina walipoanza kushindwa mwanzoni mwa vita, wakatamani
ngawira. Hivyo wakawa wameacha amri ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi
wa sallam) ili nao waweze kupata vishawishi vya kidunia.
106 03:165
107 03:152
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
34
www.ahlulathaar.com
09- Idadi dhaifu ya waislamu na udhaifu wa nguvu za kijeshi
ukilinganisha za makafiri
Allaah (Jalla wa ´Alaa) amebainisha dawa katika Kitabu Chake. Pindi
Anapotambua kuwa kuna Ikhlaasw ya kikweli kwenye nyoyo za waja, basi
Ikhlaasw hiyo natija yake itakuwa ni pamoja na kwamba itawashinda wale
wenye nguvu kuliko wao. Kwa ajili hiyo wakati (´Azza wa Jalla) waislamu
waliokula kiapo cha usikivu na utiifu chini ya mti walikuwa wametimiza
Ikhlaasw kama ipasavyo na akawasifu kwa hilo katika maneno Yake:
يم ال نيوت ميد الل ت لمدندنيم دذل يت ما د ت مكم مل م الشنجم م د يم م د م مما د قيت ت بدد ل لنقملل رمضد
"Hakika Allaah amewawia radhi waumini walipokupa kiapo cha usikivu na utiifu chini ya mti Alijua yale yaliyomo nyoyoni mwao"108,
ndipo Akabainisha kuwa kwa Ikhlaasw hii itawapelekea ikiwa ni pamoja na
kwamba itawafanya waweze yale ambayo hapo kabla walikuwa si wenye
kuyaweza. Amesema (Ta´ala):
م ت ل م ـ مل يمقللدرت ا م مييل ما قملل موماام ال نيوت بدما
"Na [atakupeni ngawira] nyingine hamjaweza kuzipata bado [ambazo] Allaah amekwishazizingia."109
Amesema wazi kwamba wasingeyaweza hapo kabla. Lakini Yeye ndiye
ameyazunguka na akawafanya kuweza. Kwa hivyo akayafanya kuwa ni
ngawira kwao pale alipojua Ikhlaasw waliokuwa nayo nyoyoni mwao. Siku
moja pindi makafiri walipowashambulia waislamu katika vita vya Ahzaab
ambapo waliwazingira kwa nguvu za kijeshi. Amesema (Ta´ala) kuhusu tukio
hilo:
يم الل ت لمدنت نم ل نيود الظبنت وم ىتنمالدكم ابيل ت د مبلصمارت مبيم م م د اللقت ت ت اللمنماجد م م مظتنب نم د فم م مدن ت ل م دذل زما م د األل دذل جماءت ت مد ي يم لقد ت ل ممديل مال
ا مزتللندلت ا زدللنما ن ملد لن
108 48:18
109 48:21
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
35
www.ahlulathaar.com
"Walipokujieni kutoka juu yenu, na kutoka chini yenu, na macho yalipokodoka, na nyoyo zikafikia kooni [kwa woga] na mkamdhania Allaah dhana mbalimbali [zisizo nzuri]. Hapo ndipo waumini walipojaribiwa na wakatetemeshwa tetemesho kali kabisa."110
Wakati huo ilikuwa kutibu udhaifu huu na uzingiraji wa kijeshi ni kwa kumtakasia nia Allaah na kumuamini kwa imani ya nguvu. Amesema (Ta´ala):
ا مما م ملموم ال نيوت مرمات لتوت م ملمقم ال نيوت مرمات لتوت يـ م نما م قمالت ا ىم مول ممما زما مىت ل د ن ديماون م مسل دي نا ملم نا رم م الل ت لمدنت نم األل
"Basi waumini walipoona yale makundi, walisema: “Haya ndio yale Aliyotuahidi Allaah na Mtume Wake na amesema kweli Allaah na Mtume Wake" na haikuwazidishia isipokuwa imani na kujisalimisha zaidi.""111
Ikhlaasw hii ikapelekea ikiwa ni pamoja na yale Allaah aliyoelezea:
ييل نا م مانم ال نيوت قم د مند ننا م م نملم الن د يم ظماىم ت ىت مد يل مىل د م مفم ال نيوت الل ت لمدندنيم اللقد مالم مرم ن ال نيوت الن د يم مفم ت ا بد ميلظد د ل مل يمنمالت ا مرمىت ل م ممل ماآمت ل م مرلضنا نل ي د ل مقم مفم د قيت ت بدد ت ال ب ليم م د قنا يمقل يت ت نم م ملاد ت نم م د قنا م م لرم م ت ل مرلضم ت ل م د م الل د ما د مدي ميما د
ا ءء قملد نا مطم ت ىم م مانم ال نيوت م م ـ ت د ميل
"Allaah akawarudisha nyuma wale waliokufuru kwa chuki zao hawakupata kheri yoyote na Allaah amewatosheleza waumini vitani. Na Allaah ni Mwenye nguvu kabisa, Mwenye enzi. Na Aliwateremsha wale waliowasaidia [maadui] miongoni mwa Ahl-ul-Kitaab kutoka katika ngome zao na Akatia khofu katika nyoyo zao; kundi mnaliua na kundi jingine mnaliteka. Na Akakurithisheni ardhi yao, na majumba yao, na mali zao na ardhi hamkuwahi kuzikanyaga. Na Allaah daima juu ya kila kitu ni muweza."112
Hawakuwa wakifikiria kuwa Allaah atawasaidia kwa njia hiyo, nayo ni kwa Malaika na upepo:
م م يب ما الن د يم ممنت ا اذل ت ت ا د ل م م ال نيود م ميل ت ل دذل جماءم ل ت ل جتنت ه م مرلام لنما م ميل د ل ردينا مجتنت نا نل يم م لىما
110 33:10-11
111 33:22
112 33:25-27
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
36
www.ahlulathaar.com
"Enyi mlioamini! Kumbukeni neema ya Allaah juu yenu pale yalipokujieni majeshi Tukawapelekea upepo wa dhoruba na majeshi msiyoyaona."113
Miongoni mwa dalili zenye kuonesha kuwa Uislamu ndio dini ya haki, ni kuwa umati mdogo wa watu na ulio dhaifu ulioshikamana na Uislamu unashinda umati mkubwa na wenye nguvu wa makafiri:
مال نيوت ممعم الصنابد د يم م مد ي د م ء قم دي م ء م م م ل د م ن م د م ن ددذلند ال نيود
“Makundi mangapi machache yameshinda makundi mengi kwa idhini ya Allaah? Na Allaah yu pamoja na wenye kusubiri.”114
Kwa ajili hiyo ndio maana Allaah (Ta´ala) akaita siku ya Badr kuwa ni
"alama", "hoja" na "pambanuzi" kwa sababu imetolea dalili kuonesha kuwa
Uislamu ndio dini ya haki. Amesema (Ta´ala):
د الل يمقم ما د م ه يتقما د ت د ام دي د ال نيود م ت ل م ـ ما د م ه قملل مانم لم ت ل م ه د د يم يمنيل
"Kwa hakika ilikuwa ni alama kwenu katika makundi mawili yalipokutana. Kundi linapigana katika njia ya Allaah na jingine kafiri."115
Hapa ilikuwa siku ya Badr.
ل نيود ممما م نمللنما م م ـ م للدوم يم لمم اللفت لقماند دن تن ت ل ممن ت د
"Ikiwa nyinyi mumemwamini Allaah na yale Tuliyoyateremsha kwa mja Wetu siku ya Upambanuzi."116
Ilikuwa siku ya Badr.
لد ييم ل دكم مميل ىم مكم مي بميد نم ء ميمل مـ مميل ومين مي بميد نم ء
"Ili aangamie yule wa kuangamia kwa hoja bayana na ahuike mwenye kuhuika kwa hoja bayana."117
113 33:09
114 02:249
115 03:13
116 08:41
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
37
www.ahlulathaar.com
Kadhalika ilikuwa siku ya Badr kwa mujibu wa baadhi.
Umati mdogo na dhaifu wa waumini kushinda umati mkubwa na wenye
nguvu wa makafiri, bila ya shaka ni dalili ya kwamba umati mdogo huu uko
juu ya haki na kwamba ni Allaah ndiye ambaye kaunusuru. Amesema katika
vita vya Badr:
رء م م ت ل مذدلن ه ملمقملل مصم م ت ت ال نيوت بد ملل
"Kwa hakika alikunusuruni Allaah katika Badr na hali nyinyi mlikuwa dhaifu."118
اد م د مود مم م ت ل يم م د ت ا الن د يم ممنت ا ي رمببكم د م الل م م ام تللقدي د قيت ت د الن د يم مفم ت ا ال ب ليم دذل ت ود
"Pale Mola wako alipowatia ilhamu Malaika [kuwaambia]: “Hakika Mimi niko pamoja nanyi, basi wathibitisheni wale walioamini. Nitatia woga kwenye nyoyo za waliokufuru."119
Allaah amewaahidi waumini kuwa atawanusuru. Allaah (Ta´ala) amezitaja
sifa zao na kuwapambanua na wengine:
دنن ال نيوم لمقم د ك مند نه ملميمنصت منن ال نيوت ممي منصت تهت
"Bila shaka Allaah atamnusuru yeyote anayemnusuru. Hakika Allaah ni Mwenye nguvu kabisa, Mwenye enzi."120
Kisha akawapambanua na wengine wote kwa sifa zao:
لل م ل ت فد م يم م لا ميد الل تن م د مرلضد مقمامت ا الصن م م م يم تا النن ما م م ممم ت ا د تمت رد الن د يم دن من ننناىت ل د األل ملد نيود ماقد م ت األل
"Ambao Tukiwamakinisha katika ardhi, husimamisha swalah na hutoa zakaah na huamrisha mema na hukataza maovu. Na kwa Allaah Pekee ndio hatima ya mambo yote."121
117 08:42
118 03:123
119 08:12
120 22:40
121 22:41
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
38
www.ahlulathaar.com
Dawa hii tuliyoiashiria dhidi ya uzingiraji wa kijeshi, kadhalika ndio dawa
dhidi ya uzingiraji wa kiuchumi. Allaah (Ta´ala) ameashiria hilo katika Suurah
"al-Munaafiquun" na kusema:
ىت ت الن د يم يمقت لت نم م تنفدقت ا م م ـ مميل دنلم رمات لد ال نيود وم نـ منفميب ا
"Wao ndio wale wasemao: “Msitoe [mali] kwa ajii ya walioko kwa Mtume wa Allaah mpaka watoweke.""122
Kitendo hichi ambacho wanafiki walikuwa wanataka kuwafanyia waislamu si chengine isipokuwa ni uzingiraji wa kiuchumi. Akaashiria (Ta´ala) ya kwamba dawa yake ni kuwa na imani yenye nguvu Kwake na kuelekea Kwake (Jalla wa ´Alaa) kikweli. Amesema:
قم ت نم مرلضد ملميـ دين الل تنما دقدنيم م يمفل ملد نيود منمااديت السن ما مااد ماألل
"Na ni za Allaah Pekee hazina za mbingu na ardhi, lakini wanafiki hawafahamu."123
Ambaye mikononi Mwake mna hazina za mbingu na ardhi mtu akimuelekea, haanguki:
يت مممي يم يم م ن ل م م ال نيود يم ت م ومسل توت مممي يم ن د ال نيوم يمل م لنوت مل مجنا م يم لزتقلوت مديل وميلثت م يمل مسد
"Na yule anayemcha Allaah humjaalia njia [ya kutokea] na atamruzuku kutoka njia ambayo hatizamii. Na yule anayemtegemea Allaah, basi Yeye humtosheleza."124
Akabainisha hilo vilevile kwa kusema:
فل ت ل مييل م ن مسم لفم يت لندي ت ت ال نيوت مدي ميل دود دن ماءم م دنل د
"Na mkikhofu umasikini basi Allaah atakutajirisheni kutokana na fadhila Zake - Akitaka."125
122
63:07
123 63:07
124 65:02-03
125 09:28
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
39
www.ahlulathaar.com
10- Jamii kutofautiana nyoyo
Amebainisha (Ta´ala) katika Suurah "al-Hashr" kwamba suala hili sababu yake
ni kutokuwa na akili. Amesema:
نيم ت ل ملد له م يتقما د ت م ت ل جمدي نا د ن د قيت ن مبمصننم ء م ل مدي مرماءد جتلترء ملسم يت ت ل جمدي نا مقيت ت بيت ت ل م نـ ملات ت بيمييل
"Hawatopigana nanyi kwa mkusanyiko isipokuwa kuwa katika miji iliyozatitiwa kwa ngome au nyuma ya kuta. Uadui wao baina yao ni mkali. Utawadhania wameungana pamoja kumbe nyoyo zao zimetofuatiana."126
Kisha Akabainisha ni kwa nini mambo yako namna hiyo:
لدكم دم ين ت ل قيم لمه ن يم لقد ت نم ذمـ
"Hayo ni kwa kuwa wao ni watu wasio na akili."127
Ukosefu wa akili ni ugonjwa ambao dawa yake ni kufuata nuru ya Wahy. Wahy unaongoza katika manufaa ambayo hayawezi kudhibitiwa na akili:
ماردجء مد نيل ما ي بدود د النناسد م مي من يم توت د الظب ت مااد لميل م بد نماهت مجم م لنما لموت ت رنا يملشد ييمييل م مممي مانم ممييل نا م مول
"Je, aliyekuwa maiti kisha Tukamhuisha na Tukamjaalia nuru anatembea kwayo kati ya watu, ni sawa na yule ambaye yumo katika viza si mwenye kutoka humo?"128
Hapa Amebainisha kuwa nuru ya imani inamuhuisha yule ambaye ni maiti na unamwangazia njia anayopitaeko. Amesema (Ta´ala):
ب الن د يم ممنت ا يتل دجت ت مد يم الظب ت مااد د م النب رد ال نيوت م د
"Allaah ni kipenzi wa wale walioamini - Anawatoa kutoka katika viza na kuwaingiza katika nuru."129
ي ام د م م ـ د مااء مبسل مقدي ء لم ـ ممني يملشد ي مت د ا م م ـ مجل دود مىل م م مي يملشد
126 59:14
127 59:14
128 06:122
129 02:257
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
40
www.ahlulathaar.com
"Je, yule anayekwenda akisinukia juu ya ya uso wake ni mwongofu zaidi au yule anayekwenda sawasawa kuelekea njia iliyonyooka?"130
Kwa ufupi manufaa haya ya kibinaadamu yanayojenga nidhamu za kidunia yanazunguka katika aina tatu:
Ya kwanza: Kuzuia madhara. Madhara haya kwa wanachuoni yanajulikana
kama "mambo ya kidharurah". Yanahusiana na kuzuia madhara katika nyanja
sita tulizozitaja kabla:
1- Dini.
2- Nafsi.
3- Akili.
4- Nasabu.
5- Heshima.
6- Mali.
Ya pili: Kufikia manufaa. Manufaa haya kwa wanachuoni yanajulikana kama
"haja". Katika matawi yake ni biashara na deni kwa mujibu wa maoni
yanayoonelea hivo. Kadhalika inahusiana na manufaa mengine yote ya
kubadilishana baina ya watu katika jamii kwa njia ya Kishari´ah.
Ya tatu: Kujipamba kwa tabia na desturi nzuri. Katika vitaga vyake ni zile sifa
za kimaumbile kama kuziachia ndevu, kuyapunguza masharubu, uchafu wa
haramu na kuwapa riziki ndugu mafukara.
Hakuna yeyote wala chochote kinachohifadhi manufaa haya kwa njia ya
hekima na nzuri zaidi kama Uislamu:
د ما ه تول د م ل م توت ثتن تصد م ل مدي لنلتنل وم دي ء م د ء ال
"Alif Laam Raa. Hiki ni Kitabu ambacho Aayaat Zake zimetimizwa barabara kisha zikapambanuliwa vyema kutoka kwa Aliye na hikmah na Mwenye ujuzi wa kila kitu."131
130
67:22
131 11:01
Uislamu ni dini iliyokamilika
ash-Shanqiytwiy
41
www.ahlulathaar.com
Swalah na salaam zimwendee Muhammad, kizazi chake na Maswahabah zake
wote.
Top Related